Mekhissi-Benabbad anawapungua watu mikono akiwa na shati lake mdomoni

Mwanariadha wa Ufaransa, Mahiedine Mekhissi-Benabbad amepokonywa medali yake ya dhahabu, aliyotarajiwa kuipata baada ya kushinda mbio za mita 3,000 za kuruka viunzi, katika mashindano ya riadha barani Ulaya.

Kilichomkuta mwanariadha huyu kilitokana na hatua yake ya kuvua shati lake alipokuwa anaelekea kushinda mbio hizo.
Mekhissi-Benabbad alivua shati lake na kuliweka kinywani pindi tu alipovuka msitari na kuibuka mshindi katika mbio hizo.

Awali, alionekene kupewa kadi ya manjani kama onyo na mmoja wa maafisa wa mashindano hayo ila hatimaye alipokonywa ushindi wake.
Mekhissi-Benabbad baada ya kutoa shati lake na kujifunika bendera ya ufaransa

Post a Comment

 
Top