Wananchi nchini Nigeria wameandamana na kuitaka serikali ya Rais Goodluck Jonathan kutoeneza machafuko katika maeneo ya kaskazini mwa nchi hiyo. 

Matamshi hayo yametolewa kwenye maandamano yaliyofanyika katika mji mkuu Abuja kupinga kutekwa nyara wanafunzi wasichana wa shule na kundi la kitakfiri la Boko Haram.

Oby Ezekwesili, mratibu wa kampeni ya ‘Warejesheni Wasichana Wetu’ amesema Rais Jonathan anapaswa kuangalia upya stratejia za serikali katika kukabiliana na ugaidi Nigeria. 

Ameongeza kuwa, ni muhimu kwa rais huyo Amiri jeshi mkuu wa jeshi kujadiliana na timu ya usalama na kuangalia tena stratejia za operesheni hiyo.

Maandamano hayo yamefanyika wakati siku ya Alkhamisi watu wenye silaha walishambulia kijiji cha Gurmushi kaskazini mwa Nigeria na kuua watu wasiopungua 32.

Rais Goodluck Jonathan alitangaza siku hiyo pia kuwa ameamuru kufanywa operesheni kali dhidi ya kundi la Boko Haram na kuvitaka vikosi vya usalama kuchukua kila hatua kuhakikisha kwamba kundi hilo linasambaratishwa.

Tehran.

Post a Comment

 
Top